Jumapili, 6 Machi 2016

Maelfu ya wakimbizi kutoka Msumbuji wamiminika Malawi,baada ya kuzuka kwa mapigano ya kisiasa

HABARI KUTOKA MALAWI NA EPHRAIM MKALI BANDA.

Picha hawa ni baadhi ya wakimbizi hao kutoka Msumbiji wakiwa katika picha tofauti





Nchi ya Malawi imewapokea wakimbizi wengine zaidi ya 8000 kutoka inchi ya Msumbiji,  Wananchi hao raia wa Msumbiji wana kimbia nchi yao baada yakuzuka mapigano ya kisiasa kati ya wafuasi wa chama tawala cha Frelimo na Renamo, chama cha Renamo hakikubaliani na matokeo ya uchaguzi ambayo yalitangazwa nchini humo.

Idadi hiyo ime thibitishwa na shirika la kuhudumia wakimbizi duniani (UNHCR). Shirika hilo limeipongeza serikali ya Malawi kwa kua pokea wakimbizi hao,

Pia Shirika hilo limetoa tahadhari dhidi ya magonjwa ya mlipuko ambayo yanaweza tokea kutokana na kuwepo kwa idadi ya watu wengi katika kempu ya Kapise iliyopo katika wilaya ya Mwanza mpakani na Msumbiji.

Umoja wa mataifa umesema Dola milion kumi na tano (kwacha Trillion moja ya Malawi) inahitajika ili wakimbizi hao waweze kupewa msaada wa kutosha.

Nao mabalozi wa nchi za Ujerumani na Brazil balozi Peter Woesta na Gustavo Nogueira walio tembelea kempu hio kujionea hali halisi ya wakimbizi.

UNHCR imeiomba serikali ya Malawi kufikiria namna ya kuongeza eneo lingine kwa ajili ya wakimbizi ambao wana endelea ku miminika katika nchi hio.


Serkali ya Malawi imesema inafikilia ombi hilo. Takribani wakimbizi elufu shirini na tano kutoka Msumbiji wanahifadhiwa nchini Malawi. Watu wengine wamesema Umoja wa Africa unatakiwa kuangalia hali inayotokea kwa sasa Msumbiji kwa upana zaidi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni