Jumatatu, 19 Desemba 2016

BANDARI YA DAR ES SALAAMA KUKOSA REKODI ZA TAKA NI UDHAIFU MKUBWA- MPINA

NA EVELYN MKOKOI – DAR ES SALAAM
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira  Mh. Luhaga Mpina akizungumza na Viongozi wa Bandari ya Dar es salaam mara baada ya kuwasili Bandarini hapo kwaajiri ya kufanya ziara.

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mzingira Mhe. Luhaga Mpina amefanya ziara ya kushtukiza katika bandari ya Dar es salaam ili kujionea utaratibu wa Bandari hiyo wa kuondosha taka zitokanazo na shughuli zake.

Ziara ya Naibu Waziri Mpina imetokana na Malalamiko ya wananchi yaliyodai kuwa uchafuzi mwingi umekuwa ukifanyika katika Bahari na sehemu kubwa ya fukwe ya bandari imekuwa ikijaa taka za aina mbali mbali.

Kutokana na malalamiko hayo ya wakazi wa jiji la Dar es Saalam, Naibu Waziri kabla ya kukagua maeneo ya kutoa na kukusanya taka za aina mbali mbali katika bandari hiyo zikiwemo taka za mafuta ghafi, alipokea taarifa kutoka kwa uongozi wa Bandari ambapo ameshangazwa na kile kilicholezwa na Afisa Mazingira wa bandari Bwana Thobias Sonda kuwa Bandani hiyo kubwa katika kanda ya Afrika Mashariki haina sehemu ya kupokea taka yaani waste reception facility na haina takwimu za taka zinazoingia na kutoka Bandarini Hapo.

Akishindwa kujibu baadhi ya maswali yaliyoulizwa na Naibu Waziri Mpina Afisa mazingira huyo alieleza kuwa, Bandari hiyo inazalisha aina mbili kubwa za taka ikiwa ni taka za aina mbali mbali na taka za maji taka, alisema kuwa taka hizo zinaondoshwa na wakala ambao wanasajiliwa na Sumatra lakini haikueleweka wazi kuwa, taka hizo zinatupwa wapi na aliongeza kwa kusema kuwa, taka nyingi na hali ya uchafu inayoonekana pembezoni mwa Bandari ya Dar es Salaam inatokana na shughuli za kibinadamu kiwandani hapo, na kusema kuwa, kuna utaratibu wa kufanya usafi na kuziondosha na kukanusha kuwepo kwa taarifa za boat na meli zinazofanya safari za kuanzia bandarini hapo kuchafua mazingira ya bandari na Bahari.

Afisa Mazingira huyo, liongeza kwa kusema kuwa taka za maji taka pamoja na kukosekana kwa takwimu za uondoshwani na umwagaji, zimekuwa zikikuswanywa na magari yao maalumu na kumwagwa katika mabwawa yao yaliyopo Kurasini jijini Dar es Salaam.

Kwa kushangwazwa na hali hiyo, Mpina kupitia Baraza la taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira NEMC ameutaka uongozi wa Bandari hiyo kujenga mfumo mzuri wa kuhifadhi taka kwa muda wa miezi sita na kuripoti kwa Baraza za Mazingira kwa miezi mitatu Mfulizo kuonyesha namna ambavyo uondoshaji wa taka hizo unafanyika, Pamoja na kuwasilisha ripoti kwa Baraza ya  Namna ambavyo mawakala hao walipatikana.

Aidha Naibu waziri Mpina ameliagiza baraza kumpelekea ripoti  ndani ya siku saba, inayoonyesha kama hao mawakala wa kukusanya taka bandarini wapo kisheria.

Kwa Upande wake Kaimu Meneja wa Mamlaka ya Bandari Nchini Bw. Nelson Mlele amesema kuwa amepokea maagizo ya Mhe kupitia NEMC kwani yanawakumbusha utekelezaji wa majukumu yao na kwa upande wa Bandari ni changamoto itakayofanyiwa kazi haraka.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni