Ijumaa, 27 Mei 2016

Kundi la kiharifu linalo ongozwa na vijana almaarufu kama "teleza" lazuka huvamia nyumba za wanawake na kuwabaka!!

Wananchi wa Mtaa wa Simu Manispaa ya Kigoma Ujiji wakiwa wamekusanyika nyumbani kwa Mwenyekiti wa mtaa huo, Tausi Issa wakishinikiza kukomeshwa vitendo vya ubakaji kwa wanawake vinavyofanywa na vijana wanaofahamika kwa jina la Teleza jana. (Picha na Fadhili Abdallah).
Wananchi wa mtaa wa simu manispaa ya Kigoma ujiji wakiwa wamekusanyika nyumbani kwa mwenyekiti wa mtaa huo Tausi issa wakishinikiza kukomeshwa kwa vitendo hivyo.
Mapema wiki hii hali ya sintofahamu ilizuka kwa wakazi wa  maeneo kadhaa ya katika Manispaa ya Kigoma Ujiji baada ya kuibuka kwa kundi la kihalifu la vijana alimaarufu kama teleza ambao huvamia nyumba ambazo huishi wanawake na kuwabaka nyakati za usiku

Inadaiwa vijana hao maarufu kama teleza, hujipaka mafuta ya mawese kabla ya kuvamia nyumba za ambazo huishi wanawake pekee kisha kutenda uhalifu huo.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa Kigoma, Ferdinand Mtui alithibitisha kuwapo matukio hayo na kusema tayari jeshi la polisi limemkamata mtuhumiwa mmoja baada ya kuwahoji wanawake nne (4) waliofika kituo kikuu cha polisi kutoa malalamiko ya kuingiliwa katika nyumba zao na vijana hao.

Hata hivyo, Kamanda Mtui aliwatoa wasi wasi wakazi wa Manispaa ya Kigoma Ujiji akieleza kuwa vitendo vinavyofanywa na vijana hao havihusiani kwa namna yoyote na vitendo vya kishirikina.

Alisema wanaoviendesha ni watu halisi ambao wameamua kufanya vitendo hivyo na polisi imeanza kuchukua hatua madhubuti za kupambana navyo.

Inaelezwa kua kufuatia hali hiyo kundi la wanawake walikusanyika kwa Mwenyekiti wa Mtaa wa Simu Kata ya Mwanga Kusini wakishinikiza serikali kuchukua hatua.

Ambapo katika maelezo yao walidai kua tayari wanawake wanne walijeruhiwa miili yao kwa silaha ambazo wabakaji hao wamekuwa wakitembea nazo baada ya kuvamia nyumba zao.


Diwani wa kata ya Mwanga Kusini, Mussa Maulid alikiri kupokea malalamiko ya wanawake 12 wanaodai kuingiliwa na vijana hao maarufu kama teleza.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni