Ijumaa, 3 Juni 2016

Zaidi ya watu 140,000 Wilaya ya Monduli wanatarajiwa kupata tingatiba ya ugonjwa wa trakoma (vikope).

Na.Catherine Sungura-Monduli
Mkuu wa Wilaya ya Monduli Francis Miti akihutubia wanakijiji wa kijiji cha Meserani juu(hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa umezaji kingatiba ya ugonjwa wa vikope(trakoma),kulia ni Mratibu wa Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Magonjwa Yaliyokuwa Hayapewi Kipaumbele toka Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamio,Jinsia,Wazee na Watoto,Dkt.Upendo Mwingira


Wilaya ya Monduli inatarajia kutoa kingatiba ya ugonjwa wa trakoma(vikope) kwa watu wapatao 140,962 kwa ngazi ya jamii  kaya kwa kaya hadi ifikapo mwezi julai mwaka Huu

Haya yamesemwa leo na mkuu wa wilaya ya Monduli Fransic Miti wakati wa uzinduzi wa zoezi la ugawaji dawa katika kijijo cha Losingirani. 

Miti alisema kila mtu yupo katika hatari ya kupata maambukizi ya magonjwa yaliyokuwa hayapewi  kipaumbele"napenda kusisitiza kila mwanajamii ahakikishe kila mtu katika familia anatumia dawa hizi ili tuweze kupunguza kasi ya maambukizi ambayo ni tayari  katika jamii yetu.

Aidha aliahidi kulisimamia zoezi hilo ipasavyo katika ngazi zote kwani vifaa vyote vya utekelezaji wa zoezi hili vimeshawafikia katika wilaya Nzima.

Mkuu wa Wilaya alisema kwa mwaka uliopita wilaya yake imetekeleza zoezi la ugawaji wa  dawa za kudhibiti magonjwa ya kichocho  na minyoo ya tumbo kwa watoto wenye umri wa kwenda shule kwa ufanisi mkubwa ambapo kati ya watoto 29,427,watoto 28,205 walipatiwa kingatiba ambayo ni sawa na asilimia 95.8

Hata hivyo alisema kwa zoezi la mwezi wa tano mwaka huu la umezaji dawa za minyoo zilitolewa kwa watoto 31,150 sawa na asilimia 97.3 kati ya watoto 32,000.

Naye Mratibu wa Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Magonjwa Yaliyokuwa
Hayapewi kipaumbele toka Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt.Upendo Mwingira alisema maambukizi ya ugonjwa wa vikope(trakoma) upo kwa kiwango cha juu kwenye maeneo ya wafugaji ambapo asilimia 57 ya watu waliofanyiwa utafiti mwaka 2004 hadi 2006 ilionesha wana tatizo la vikope hasa wilaya ya Monduli,Longido pamoja na Ngorongoro.

inakadiliwa hadi kufikia mwaka 2020 dunia nzima iwe imetokomeza ugonjwa huu kwa kugawa dawa ambazo ni tiba na kinga.

Mwenyekiti wa kijiji cha Meserani juu,Ngimasirwa Silalee akimeza dawa kwenye uzinduzi huo,kulia ni mkuu wa wilaya ya monduli
Wananchi wa kijiji cha Meserani wakisikiliza hotuba toka mkuu wa wilaya (hayupo pichani) wakati wa uzinduzi wa umezaji wa kingatiba za ugonjwa wa trakoma uliofanyika kwenye kitongoji cha Losingirani
Diwani wa kata ya Meserani Mhe.Loti Naparana akimeza kingatiba ya Trakoma(Zithromax)wakati wa uzinduzi huo
Mama wa boma bi.Himayo Merio (aliyeshika kikombe)akipokea kingatiba toka Kwa mhudumu wa afya ngazi ya jamii bi.Jamila Karanga.zoezi hili linafanyika katika jamii hiyo kwa kuwatembelea kaya kwa kaya
Mmoja wa mtoto katika boma la mzee Sanare  Midimi wa kitongoji cha Losingirani akinyweshwa dawa iliyopo kwenye mfumo wa maji maalum kwa watoto wadogo(Picha zote na Catherine Sungura-Wizara ya Afya)
Dkt.Upendo Mwingira(mwenye nguo burgundy) akimpatia kingatiba Mkuu wa Wilaya ya Monduli Francis Miti
Kikundi cha ngoma cha akina mama wajasiriamali cha kimasai wa kijiji hicho wakitumbuiza wakati wa uzinduzi wa umezaji wa kingatiba ya Trakoma

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni