Ijumaa, 3 Juni 2016

Imani za kishirikina zapelekea vitendo vya ubakaji na ulawiti dhidi ya watoto kushamiri mkoani Iringa


Kufuatia kukithiri kwa vitendo vya ubakaji mkoani iringa, serikali imelazimika kuwagiza  wazazi za walezi kuto ruhusu watoto wenye umri chini ya miaka 14 kutembea mitaani haswa nyakati za jioni kuanzia saa 12 jioni.

Rai hiyo imetolewa na mkuu wa wilaya ya Iringa ndugu Richard Kasesela, ambapo amesema kua wazazi na walezi wana jukumu la kuwalinda watoto dhidi ya ukatili ambao unakua kwa kasi mjini Iringa.

Inaelezwa kua watekelezaji wa matukio hayo ya ukatili dhidi ya watoto kama ubakaji na ulawiti wamekua wakitumia mbinu ya kuwahadaa watoto kwa kuwapa kiasi kidogo cha pesa ama kujifanya wakiwatuma katika maeneo ambayo ni rahisi kwenda kuwafanyia ukatili huo.

Wiki moja iliyopita wananchi walimpiga hadi kumuua kijana aliyefahamika kwa jina moja la Emmanuel (25-30), baada ya kukutwa akimbaka mtoto mwenye umri wa miaka kumi, katika eneo la Mtwivila, Manispaa ya Iringa.

katika kipindi cha miezi mitatu kumeripotiwa matukio zaidi ya 30 ya ubakaji katika Manispaa ya Iringa huku watuhumiwa kumi na saba (17) wakiwa wamekamatwa na kutiwa mbaroni

Kasesela amesema matatizo ya ubakaji na uwalawiti watoto yamekuwa sugu hivyo hili kukomesha hali hiyo  ushirikiano baina ya polisi, wananchi na viongozi wa serikali na dini unahitajika ili kukomesha hali hiyo.

Kwa upande wake Naibu Meya wa Manispaa ya Iringa ndugu Joseph Lyata  amesema tatizo la kushamiri kwa vitendo ya ubakaji na ulawiti vinachangiwa na imani za kishirikina,

Alisema katika uchunguzi uliofanywa ulibaini kuwepo kwa imani za kishirikina baada ya kubaini kumekua na vikaratasi vilivyokuwa vikisambazwa mitaani vikishauri wanaume kujihusisha na vitendo hivyo vya kikatili sambamba na kujiunga na freemason ili  kufanikiwa kimaisha.

“Mtaa wa Semtema ndiyo ulikuwa tishio na huko tuliokota vikaratasi vilivyokuwa vimeandikwa ukitaka kutajirika, jiunge na freemason pia ubake au kulawiti mtoto chini ya miaka 14,” alisema.

Lyata alisema sababu nyingine ni ulevi wa kupindukia na utumiaji wa dawa za kulevya kama bangi.

Alisema kukithiri kwa vitendo hivyo kumeifanya manispaa hiyo kutangaza jambo hilo kuwa ni janga ambalo lazima wapambane nalo kwa kuwasaka wabakaji.

Aliongeza kua vitendo vya ulawiti na ubakaji vimekua vikifanywa hata majumbani na kwamba kufuatia hali hiyo serikali imeanza kuawambua wtoto wa mitaani na kuwarudisha majumbani kwao ili kuwanusu na vitendo hivyo. 

Mmoja kati ya wananchi aliejitambulisha kwa jina la Gerald Matibabu alisema kwa upande wao wananchi sasa wamekua wakijichukulia sheria mkononi kwa kuwa ua wale wote wanaobainika kujihusisha na vitendo ubakaji na ulawiti.

Hata alisema  wamelazimika kujichukulia sheria mkoni kwa kua watuhumiwa wamekua wakiachiwa huru na polisi na kurejea mtaani jambo ambalo linawaumiza sana wananchi 

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Iringa, John Kauga alikiri kuwapo kwa vitendo vya ulawiti na ubakaji na kuwataka wananchi kutoa taarifa haraka vinapotokea.

“Kuna matukio mengi pia majumbani, wazazi wasifiche, watoe taarifa kwa polisi ili hatua kali za kisheria zichukuliwe,” alisema.


Aliwataka wananchi kupinga imani za kishirikina zinazowahamasisha kufanya ukatili kwa watoto kwa madai ya kutajirika.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni