Jumamosi, 17 Desemba 2016

Mbunge Sugu "sikukimbia baada ya ajali" kilichotokea ni........!!!!

Mbunge Joseph Mbilinyi (SUGU), akizungumza na wanahabari mkoani Mbeya kuhusu ajali hiyo.

Gari la mbunge Joseph Mbilinyi (SUGU) baada ya kupata ajali.
Gari la polisi linalotumiwa na askari wa usalama barabarani (trafik) katika eneo la tukio Isanga (barabara ya Chunya) Mbeya.
Gari la Mbunge wa Mbeya mjini Joseph Mbilinyi maarufu kwa jina la Sugu, limepata ajali na kusababisha kifo cha mtoto wa miaka 13 mwanafunzi wa shule ya sekondari Lupato.

Ajali hiyo imetokea jana asubuhi majira ya saa 2:00 asubuhi ambapo gari lenye namba za usajili T161 CPP mali ya mbunge wa Mbeya mjini Joseph Mbilinyi ambalo lilikuwa likiendeshwa na Gabriel Andrea (43) mkazi wa Mwakibete, lilifeli break na kusababisha kifo cha mtoto Rahel/Rachael  Lutumo ambae alikuwa akivuka bara bara Iyunga katika eneo la kuvukia watembea kwa miguu (zebra).

Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya kaimu kamishna Dhahir Kidavashari, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba mtoto Rahel Lutumo alifariki njiani wakati akikimbizwa Hospital ya Rufaa Mbeya kwa ajili ya kupatiwa matibabu na mwili wake kuhifadhiwa katika hospital ya Rufaa Mbeya na kwamba dereva wa mbunge Sugu anashikiliwa na jeshi la polisi kwa mahojiano zaidi.

Kwa upande wake mbunge Joseph Mbilinyi  maarufu kwa jina la SUGU ambae hakuwa tayari kuzungumza na wanahabari ili kuizungumzia ajali hiyo amesema amesikitishwa na ajali hiyo ambayo imepoteza maisha na mwananchi ambae hana hatia.

Akizungumzia madai ya gari lake kukimbia eneo la tukio baada ya kusababisha ajali hiyo jambo ambalo lilipelekea gari lake kufukuziwa na madereva bodaboda na hatimae kurudi eneo la tukio , Mbunge huyo amekanusha  madai hayo na kusema kuwa sababu iliyopelekea kushindwa kusimama mara baada ya tukio hilo ni kutokana na gari lake kufeli break hivyo haikuwa rahisi kusimama na si vinginevyo.

Wakati huohuo askari wa nne wa usalama barabarani wamenusulika kifo baada ya  gari walilokuwa wakilitumia kupinduka  katika eneo la Isanga (bara bara ya kuelekea Chunya)
Gari hilo lilikuwa likijaribu kuwahi eneo la tukio Iyunga eneo  ambalo mtoto Rahel Lutumo aliyegongwa na gari la mbunge Sugu na kufariki dunia wakati akipelekwa hospital kupatiwa matibabu.

Akielezea ajali hiyo Kamanda wa polisi  kaimu kamishna Dhahir Kidavashari amesema chanzo cha ajali hiyo ni utelezi ambao ulisababishwa na mvua iliyokuwa ikinyesha ambapo aliwataja askari ambao wamenusurika kifo katika ajali hiyo kuwa ni askari mwenye namba F 7294 CPL Godfrey, F 2211 CPL Filbert, G 1346 PC Mwamed na G 8678 PC Shabani ambae ndiye alikuwa dereva. 

Kamanda wa polisi Dhahir Kidavashari akifafanua kuhusu ajali mbili tofauti zilizotokea mkoani Mbeya.

Gari la Mbunge Sugu. 


Gari la polisi linalotumiwa na askari wa usalama barabarani katika eneo la tukio Isanga (barabara ya Chunya) Mbeya.

Gari la polisi linalotumiwa na askari wa usalama barabarani likikokotwa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni