Jumatatu, 5 Desemba 2016

Mwanafunzi darasa la 5, aliekuwa amehamishwa shule kutoka kijijini kwenda mjini, amejinyonga.!!,


Mwanafunzi wa darasa la tano katika shule ya msingi Kizota Manispaa ya Dodoma, Yassin Abdallah (13) amejinyonga kwa kutumia shuka la bafuni baada ya kupata matokeo mabaya ya mitihani yake ya mwisho wa mwaka.


Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Dodoma, Ernest Kimola, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambalo lilitokea siku tatu zilizopita majira ya mchana katika mtaa wa Kizota Relini, Manispaa ya Dodoma.

Kwa mujibu wa Kamanda Kimola amesema baba mzazi wa marehemu Hassan Juma mwenye umri wa miaka 53 aligundua kuwa mwanae amejinyonga kwa kutumia shuka,
Nae diwani wa Kata ya Kizota, Yaredi Jamal, amesema siku ya tukuo alikuwa kwenye kikao akapokea simu kutoka kwa mwenyekiti wa mtaa akimtaarifu kuwa mwanafunzi huyo amejinyonga, na kuongeza kuwa kwa mujibu wa wazazi wa mtoto huyo, alikuwa ana miezi miwili tangu ahamie katika shule hiyo akitokea  mkoani Kigoma.

Inadaiwa mtoto huyo katika matokeo yake ya mwisho alishika nafasi ya 128 kati ya wanafunzi 132, hali ambayo ilimstua na kuamua kujinyonga
“hapo shuleni kaanza masoangemo mwezi wa 11 kwa mujibu wa walimu, ambapo kila akifundishwa na walimu alijiona haelewi kutokana na kuwakuta wenzake wakiwa wamemtangulia katika masomo wanayofundishwa,” alisema diwani Jamal.

Kufuatia hali hiyo, Diwani Jamal alitoa rai kwa wazazi kuwa karibu na watoto wao na kuepuka kutoa vitisho ambavyo vitawasabisha wachukue maamuzi magumu.

“Nimeongea  na wazazi wanasema hawajawahi kuzungumza lolote na walitambua mtoto wao anatoka kijijini anakuja kukutana na watoto wa mjini ambao uelewa wao ni tofauti, Walitarajia hadi mwakani mtoto wao angekuwa ameanza kuelewa masomo aende sawa na wenzake,” alisema Diwani Jamal.


Diwani Jamal alisema tukio hilo limemsikitisha na halijawahi kutokea mtoto mdogo kufikia uamuzi wa aina hiyo, hivyo ni vyema wazazi wakawa karibu na watoto wao kitaaluma.

chanzo: Nipashe

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni