Jumapili, 8 Mei 2016

Hila mbaya imewaponza Wafanyabiashara, Rais Magufuli asema "hawatapewa leseni ya kuagiza sukari kutoka ng'ambo badala yake serikali ndio itawajibika"


Rais wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amesema badala ya kuwapa wafanyabiashara leseni ya kuagiza sukari kutoka ng'ambo serikali yenyewe ndio itaagiza sukari hiyo moja kwa moja.
Rais Magufuli ametoa kauli hiyo baada ya kubaini uwepo wa maelfu ya tani kadhaa ya sukari ambayo ilifichwa katika mabohari katika mikoa ya Arusha na Kilombero iliyoagizwa kutoka nje na ile iliyonunuliwa kutoka kwenye kampuni za kusaga sukari nchini Tanzania.
Aidha rais amewaahidi watanzania kua katika siku zijazo sukari itapatikana kwa wingi hapa Tanzania na kuongeza kua serikali imekwisha agiza sukari na kwamba serikali haitowapa leseni ya kuagiza sukari wale wote waliowafilisi watanzania na badala yake serikali itafanaya kazi hiyo yenyewe.
''Serikali imeagiza na itauza sukari hiyo kwa bei ya chini,,,, hilo ndio lengo la serikali '' alisema rais Magufuli huku mawananchi wakimshangilia.
Hata hivyo serikali katika kuonesha kua ipo imara na haipo tayari kuyumbishwa na baadhi ya wafanyabiashara wasio na nia njema na watanzania imeanza kugawa sukari iliyoingizwa nchini kinyume cha sheria na kufichwa katika mabohari kote nchini.
TRA ilichukua hatua hiyo baada ya mwekezaji wa kibinafsi mkoani Lindi kupatikana na zaidi ya mifuko elfu tano za sukari kutoka nga'mbo.

Yamkini sukari hiyo hubadilishwa kwenye mifuko yenye nembo ya kampuni za kusaga sukari za Tanzania na kisha kuuzwa kwa bei maradufu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni