Jumatatu, 16 Mei 2016

Mchungaji wa Kanisa la Moraviani Mkoani Katavi amendishwa kizimbaji kwa koa la kuhujumu uchumi!!

Image result for meno ya tembo

Mchungaji wa kanisa la Moraviani Mkoani katavi wilaya ya Mlele katika kijiji cha Usevya Bw. Godwel Godwel Siame amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa katavi kwa kosa la Uhujumu uchumi la kukutwa na meno ya tembo yenye uzito upatao kilogramu 20 yenye jumla ya Thamani ya Tshs 90 m.

Akisoma hati ya Mashtaka mbele ya Kaimu Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Mkoa wa Katavi Mhe Chiganga Tengwa, wakili wa Serikali Jamila Mziray ameileza Mahakama kwamba Mnamo tarehe 5 mwezi 2016 Mshitakiwa Mch. Godwel alikutwa na nyara hizo zenye jumla ya Thamani ya 90 milioni zikiwa na jumla ya Uzito wa kilogramu 20.

Mahakama ilimweleza Mshitakiwa kwamba hakutakiwa kujibu lolote juu ya shitaka linalomkabili kwa kuwa mahakama hiyo haikuwa na mamlalaka ya kuendelea (Pecuniary Jurisdiction) kufuatia thamani ya nyara hizo kuwa zaidi ya Milioni 10.

Wakili aliendelea kuileza Mahakama kwamba upelelezi wa shauri hilo haujakamilika na hivyo kuomba tarehe nyingine ya kutajwa.

Mshitakiwa aliwakilishwa na wakili Msomi Patrick Amulike Mwakyusa ambae ameiomba Mahakama kuitaka Jamhuri kuleta kibali cha kuruhusu na kuipatia mamlaka Mahakama (certificate & consent) ya kuendelea na shauri hilo ili Mshitakiwa apate haki yake ya dhamana kwa kuwa kosa hilo lina dhamana.

Kesi hiyo iliyosajiliwa kwa Na EC 41/2016 imeahirishwa na kupangiwa tarehe nyingine ya kutajwa ambayo ni tarehe 23/5/2016.


Mshitakiwa amepelekwa Mahabusu mpaka tarehe iliyoamuriwa na Mahakama atakapo rudishwa tena kizimbani.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni