Ijumaa, 20 Mei 2016

Serikali yawasihi watoa huduma wa tiba asili na tiba mbadala kujisajiri!

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA WAZEE NA WATOTO

TAARIFA KWA UMMA
Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala, Wizara ya Afya ,Maendeleo ya Jamii,Jinsia Wazee na Watoto, linawatangazia waganga wote wa tiba asili na tiba mbadala wanaotoa matangazo kwenye vyombo vya habari bila kibali cha Baraza na wale wanaobadilisha kwa kutangaza kinyume na maagizo ya Baraza baada ya kupewa kibali waache mara moja. Hatua za kisheria zitachukuliwa kwa wale watakaokiuka agizo hili kuanzia siku saba (7) baada ya kutoka kwa taarifa hii.
Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala linaendelea kusisitiza watoa huduma wote wa tiba asili na tiba mbadala kujisajili, kusajili wasaidizi wao,vituo na maduka yao kabla ya mwezi wa sita. Fomu za maombi ya usajili zinapatikana kwa Waratibu wa tiba asili na tiba mbadala walipo  katika ofisi za Waganga Wakuu wa Wilaya (DMO). Waganga wote wanaotoa huduma bila kujisajili wanafanya kosa  kisheria na hatua  za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
Zingatia: Vibali vyote vya usajili na matangazo vinatolewa na Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala chini ya Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto. Vibali na usajili wa serikali hautolewi na vyama vya waganga, shirika, afisa utamaduni, polisi au mtu mwingine yeyote.
Imetolewa na
Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala

20/5/2016

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni