Jumatatu, 23 Mei 2016

Aibu msanii Nyota Ndogo aolewa na Mzungu bila kulipiwa mahari familia yagoma kwenda harusini! mwenyewe asema hajali!


Msanii Nyota Ndogo ameingia katika mgogoro na familia yake baada ya kuamua kufunga ndoa na mpenzi wake ambae ni mzungu raia wa Denmark, Mgogoro huo umewekwa bayana na kaka yake Nyota Ndogo anaejulikana kwa jina la Juma Tutu, jana tarehe 22 katika mitandano ya kijamii instagram na facebook nyota ndogo alitupia picha za tukio la ndoa yake huku akielezea hisia kutokana na furaha aliyokua nayo,

Akizungumza na Redio Citizen iliyopo nchini Kenya leo hii kaka yake Nyota Ndogo Bw. Juma Tutu amesema kua mgogoro huo ulizuka baada mzungu huyo kukataa kulipa mahari kama ilivyo ada na desturi za kiafrika mwanamke hulipiwa mahari na ndipo taratibu za kufunga ndoa hufanyika,

Katika mahojiano na kituo cha Citizen Radio kaka yake Nyota ndogo alisema yafuatayo 

“Sijui kama kuna harusi ya kiafrika ambayo inafanywa bila mahari, na hivi ninavokuelezea na mama yangu mwenyewe hakwenda harusi niko nae mimi hapa alikataa kwenda harusini sababu kubwa ya mama kukataa kwenda harusini ni yule mzungu.. yule kibabu alikataa kabisa kutoa mahari.

 maana tulimuita akakwepa kwa madai kua alikua anaenda ulaya lakini Nyota Ndogo akampigia magoti akisema oooh nioe basi bila mahari, sasa mimi kwa upande wangu niliona dada yangu kwa upande wa musiki ni international musician super star  yawezekana wanaume wanampigania yeye sasa inakuaje tena yeye anamlilia yule mzungu mzee akifikiri kwamba yule mzungu ana hela,

 basi mimi nikachukizwa sana na kitendo hicho, Nyota ndogo haambiliki hamzikizi mtu yeyotee yule babu wala nyanya wala nani akisha amua lake kasha amua ni kama ule mti wa  mlelema alivosema mzee ngala mti ameshindwa nyani kupanda ndio yeye basi, 

mimi  bifu yangu  kwenye mtandao wa kijamii kuna watu ambao hawanielewi kuna post ile niliiweka, nyota ndogo anaishi maisha ya dhiki sio ile maisha ya kuonekana kwenye tv, magazeti sijui wapi anasafiri maisha ya nyota ndogo ni mbaya sana hana kitu mama yake anateseka kabisa nilikua mimi na mama karibu siku tatu nimemwambia nyota ndogo aje tuzungumze tuyatatue haya maneno alikua anasema hajali chochote wala hajali mama wala mimi aidha twende harusini ama tusiende potelea mbali haambiliki keshakua star  yeye anajua kila kitu duniani” hayo ndio maneno ya Juma Tutu kaka yake Nyota ndogo

Wakati kaka yake akizungumza hayo Nyota Ndogo ameonekana kuto jali hali ya sintofahamu iliyopo baina yake na familia yake na kwamba amezama katika mahaba ya M Denmark huyo na badala yake amekua akiandika post katika ukurasa wake wa facebook kuelezea hisia zake juu ya furaha aliyonayo baada ya kufunga ndoa na mwandani wake huyo mzungu, 

baadhi ya post zake katika mtandao wa kijamii wa facebook Nyota Ndogo ameandika maneno yafuatayo

kweli mapenzi bahari Nikaha ilikuwa ya kufana Henning Hussein Nielsen Ndoa Ni wamuzi wa dhati toka moyoni na Nafsini. Ukipenda hunabudi kujitosa kwenye dimbwi la mapenzi.naahidi nitakuwa mke wako siku zote. 

I will always be with you forever ever.inshallah Mola atuongoze atujalie Amina. Mashallah 
‪#‎mtotowakikesimama”  huo ndio ujumbe wake huku ukichombezwa na picha hiyo hapo chini

Siku kuu katika maisha yangu ni leo nimejawa na furaha tele 
ndoa ni safari ndefu na inahitaji moyo. Nawatakieni muniombea dua zenu inshallah..Huyu ndo chaguo langu.


To love and be loved is to feel the sun from both sides.

I love my husband Henning Nielsen” huu ni ujumbe wa pili ukachombezwa kwa picha hizo hapo chini




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni